TUME YA UCHAGUZI YATEUA MRITHI WA DK. ELLY MACHA

Mbunge wa Viti Maalum Chadema, Catherine Nyakao Ruge

Na Mtapa Wilson

Tume ya Taifa ya uchaguzi leo imemteua Catherine Nyakao Ruge kuwa Mbunge wa wa Viti Maalum katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Catherine anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum akiwakilisha walemavu kupitia Chadema, Dk. Elly Macha, ambaye alifariki mwishoni mwa mwezi Machi katika hospitali ya New Cross, Wolverhamton nchini Uingereza, ambako alikuwa akitibiwa.

Kabla ya kuteuliwa kwake Catherine alikuwa mwanaharakati na masuala ya jinsia na haki za binadamu.  Lakini pia ni muweka hazina wa Chadema kanda ya Serengeti, nafasi ambayo anaishikilia mpaka sasa.
TUME YA UCHAGUZI YATEUA MRITHI WA DK. ELLY MACHA TUME YA UCHAGUZI YATEUA MRITHI WA DK. ELLY MACHA Reviewed by Unknown on 17:36 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.