TBC YAWASIMAMISHA KAZI WATANGAZAJI TISA KWA KURUSHA HABARI YA UONGO

Na Mwandishi wetu

Menejiment ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) imewasimamisha kazi watangazaji tisa wa shirika hilo, ambao walirusha hewani taarifa ya uongo kuwa Rais wa Marekani, Donald Trump amesifu utendaji kazi wa Rais Dk. John Magufuli na kwamba ni mfano mzuri wa kuigwa barani Afrika.

Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa leo na gazeti la Mwananchi, Mtendaji wa TBC, Dk. Ayub Rioba amethibitisha taarifa hiyo na kuwataja waliosimamishwa kazi kuwa ni Elizabeth Mramba, Gabriel Zacharia, Prudence Constantine, Dorothy Mmari, Ramadhani Mpenda, Leah Mushi, Alpha Wawa, Chunga Ruza na Judica Losai.

TBC ilitangaza habari hiyo ya uongo baada ya kuinukuu kutoka katika mtandao wa 'Fox-chanel.com', ambao unaodaiwa kuchapisha taarifa za uzushi kwa ajili ya kujipatia manufaa ya kibiashara na kufanya propaganda.

Mtandandao huo umewahi kuripoti kuwa Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 93.

Lakini pia hivi karibuni mtandao huo uliripoti taarifa nyingine ya uzushi kuwa Rais Magufuli amewataka wananchi wa nchi jirani ya Kenya kumuondoa madarakani Rais Uhuru Kenyatta, kwa madai ya kuwa utawala wake unawapeleka matatizoni.
TBC YAWASIMAMISHA KAZI WATANGAZAJI TISA KWA KURUSHA HABARI YA UONGO TBC YAWASIMAMISHA KAZI WATANGAZAJI TISA KWA KURUSHA HABARI YA UONGO Reviewed by Unknown on 10:54 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.