ACACIA YAKATAA KUILIPA TANZANIA DOLA BILIONI 180

Mgodi wa Buzwagi uliopo Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga.
Kampuni ya uchimbaji madini nchini, Acacia imepinga kulipa deni la dola bilioni 180 linalodaiwa na serikali ya Tanzania ikiwa ni malipo ya dhahabu na riba kutokana na kuficha kwake baadhi ya taarifa za mapato ya uchimbaji wa madini nchini.

Serikali ya Tanzania inadai deni hilo ambalo linasimamia mapato yaliyopatikana na hayakutajwa kutoka katika migodi miwili ya Buryanhulu na Buzwagi Wilayani Kahama, Mkoani Shinyanga katika kipindi cha mwaka 2000 na 2017.

Acacia ambayo ndio kampuni kubwa inayoongoza kwa uchimbaji wa madini nchini Tanzania imesisitiza kuwa imekuwa ikitangaza taarifa zake za mapato kila mara.

Taarifa hiyo imekuja kipindi ambacho tume mbili za Rais wa Tanzania, John Magufuli, ambazo zilichunguza masuala ya madini ikiwemo kiwango cha madini kilichomo kwenye mchanga unaosafirishwa kwenda nje ya nchi kuishutumu Acacia kufanya kazi zake kinyume cha sheria ikiwa ni pamoja na kukwepa kulipa kodi.

CHANZO: BBC

ACACIA YAKATAA KUILIPA TANZANIA DOLA BILIONI 180 ACACIA YAKATAA KUILIPA TANZANIA DOLA BILIONI 180 Reviewed by Unknown on 17:13 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.