GWAJIMA ATANGAZA MAOMBI MAALUMU KWA TUNDU LISSU

Sehemu ya tangazo lililoandaliwa na Kanisa la Ufufuo na Uzima kwa ajili ya kufanya maombi maalumu ya kuombea afya ya Tundu Lissu, aliyepigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa nyumbani kwake Area D mjini Dodoma.
Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima nchini, Josephat Gwajima, amesema jumapili wiki hii ataongoza maombi maalumu kwa ajili ya kuombea afya ya Tundu Lissu na kulaani vikali shambulio la risasi lililofanywa na watu wasiojulikana dhidi yake.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Gwajima imesema kwamba maombi hayo yatafanyika kanisani kwake Ubungo  jijini Dar es Salaam na kuwaomba wananchi wengine kuungana nae katika maombi hayo.

“Jumapili hii tarehe 10/09/2017, nitaongoza maombi maalumu ya kuombea afya ya Mheshimiwa Tundu Lissu na kulaani vikali kitendo cha kikatili na kinyama alichofanyiwa…..,” imesema taarifa hiyo.
GWAJIMA ATANGAZA MAOMBI MAALUMU KWA TUNDU LISSU GWAJIMA ATANGAZA MAOMBI MAALUMU KWA TUNDU LISSU Reviewed by Unknown on 16:02 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.