AFCON 2017: MISRI YAILAZA GHANA, MALI NA UGANDA WAAGA MICHUANO


Mohamed Salah
Na Mtapa Wilson

Michezo miwili imeshakwimalizika iliyokuwa inazikutanisha timu za Mali dhidi ya Uganda na Misri dhidi ya Ghana, ambapo katika mchezo wa Mali ambayo ilikuwa inalazimika kuilaza Uganda na kutumai Misiri ipoteze kwa Ghana, umeisha kwa sare pacha ya kufungana magoli 1-1.

Lakini kwa upande wa mchezo wa Misri na Ghana umemalizika kwa Misri kuilaza Ghana kwa goli moja kwa bila, ambalo limetiwa kimiani na mshambuliaji wa kimataifa wa Misri, Mohamed Salah, katika dakika ya 11.

Kwa matokeo haya sasa, timu za Misri na Ghana zimefanikiwa kufuzu na hatua inayofuata ya robo fainali na kuziacha timu za Mali na Uganda zikiaga michuano hiyo ya kombe la Mataifa huru Afrika.


AFCON 2017: MISRI YAILAZA GHANA, MALI NA UGANDA WAAGA MICHUANO AFCON 2017: MISRI YAILAZA GHANA, MALI NA UGANDA WAAGA MICHUANO Reviewed by Unknown on 21:50 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.