MOROCCO YAREJEA RASMI UMOJA WA AFRIKA

Rais wa Tanzania, Dk. John Magufuli akiwa na mgeni wake Mfalme wa Morocco, Mohammed VI, wakati alipotembelea Tanzania Oktoba 24, 2016.
Addis Ababa, Ethiopia

Jumuiya ya Umoja wa Mataifa huru Afrika (AU) imeridhia kurejea kwa Morocco katika Jumuiya hiyo baada ya kujiondoa takribani miaka 33 iliyopita kutokana na hatua ya AU kutambua jimbo la Sahara ya Magharibi kuwa mwanachama wake.

AU inatambua Sahara ya Magharibi kuwa ni jimbo huru ambalo pia ni mwanachama wake, lakini Morocco imeendelea kusisitiza kuwa eneo hilo ni mkoa wake wa kusini.

Morocco imepigania mpango wake wa kutaka kurejea tena AU mwaka uliopita, ambapo Mfalme wa nchi hiyo, Mohammed VI, alitemebelea nchi kadhaa za Afrika ikiwamo Tanzania na kufanya mazungumzo na wakuu wa nchi hizo, jambo ambalo lilielezwa kama njia ya kutafuta ushawishi wa kurejea kwake katika Jumuiya hiyo.

Eneo la Sahara ya Magharibi linaendelea kuwa eneo lenye utata mkubwa licha ya kuwa Wakuu wengi wa nchi za Afrika wamepiga kura na kuikubali Morocco kurejea katika Umoja huo katika mkutano wa AU unaoendelea mjini Addis Ababa nchini Ethiopia.

CHANZO: BBC
MOROCCO YAREJEA RASMI UMOJA WA AFRIKA MOROCCO YAREJEA RASMI UMOJA WA AFRIKA Reviewed by Unknown on 05:53 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.