RAIS MAGUFULI AKUBALI MKUU WA WILAYA KUJIUZULU


Na Mtapa Wilson

Rais John Magufuli amelikubali ombi la aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Uyuwi, Mkoani Tabora, Gabriel Simon Mnyele, ambaye aliomba kujiuzulu wadhifa wake huo kwa hiari yake mwenyewe hapo jana.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, imesema kuwa ombi la Mnyele limekubaliwa na Rais na nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Uyuwi itajazwa hapo baadaye.

Mkuu huyo wa Wilaya alimwandikia barua Rais akiomuomba ajiuzulu wadhifa wake huo jana Alhamis Januari 26, 2017 na kuwaaga madiwani wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano alioufanya wilayani humo.

Gabriel Simon Mnyele, alikuwa ni miongoni mwa Wakuu wa Wilaya 139 walioteuliwa na Rais Magufuli mnamo Juni 26, 2016.
RAIS MAGUFULI AKUBALI MKUU WA WILAYA KUJIUZULU RAIS MAGUFULI AKUBALI MKUU WA WILAYA KUJIUZULU Reviewed by Unknown on 18:23 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.