BENKI YA DUNIA KUTOA DOLA MILIONI 305 UTANUZI WA BANDARI DAR


Na Mwandishi wetu

Kutokana na matatizo mbalimbali yaliyopo kwenye bandari ya Dar es Salaam, ambayo yamekuwa yakiigharimu serikali na nchi jirani kiasi cha takribani dola za Marekani milioni 2.6 kila mwaka, Benki ya Dunia ya Dunia (WB) imesema itatoa dola milioni 305 kama mkopo, kwa ajili ya upanuzi wa bandari hiyo.

Bandari hiyo iliyoko katika jiji la Dar es Salaam, ndiyo inayoziunganisha nchi za Afrika ambazo hazipakani na bahari ya Hindi ikiwemo Zambia, Rwanda, Malawi, Burundi, Uganda na pia eneo la mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC).

Hatua hiyo imekuja kutokana na ripoti ya Benki ya Dunia iliyotolewa mwaka 2014 na kubainisha matatizo mbalimbali kwenye bandari ya Dar es Salaam na kwamba fedha hizo zitakwenda kusaidia kumaliza matatizo hayo, ambayo yalikuwa yakiigharimu kiasi kikubwa cha fedha serikali pamoja na nchi nyingine zinazotegemea bandari hiyo. 
BENKI YA DUNIA KUTOA DOLA MILIONI 305 UTANUZI WA BANDARI DAR BENKI YA DUNIA KUTOA DOLA MILIONI 305 UTANUZI WA BANDARI DAR Reviewed by Unknown on 14:55 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.