RAIS DONALD TRUMP AANZA KUWATIMUA WAAFRIKA

Rais wa Marekani, Donald Trump.
Marekani
Watu wapatao 92 wakiwamo raia 90 wa Somalia na wengine wawili wa Kenya, wamefurushwa kutoka nchini Marekani kutokana na kile kilichoelezwa kuwa walikuwa wanaishi nchini humo kinyume cha sheria.

Kwa mujibu wa Msemaji wa serikali ya Kenya, Eric Kiraithe, tayari watu hao wameshawasili katika uwanja wa Kimataifa ya Jomo Kenyatta, jijini Nairobi na raia wa Somalia watasafirishwa moja kwa moja hadi Mogadishu.

“Ni watu 90 kulingana na habari ambazo tumepewa.  Wakati unaondolewa nchi fulani kurejeshwa kwenu, huwa unarejeshwa hadi kwenu.  Kuhusu sababu iliyowafanya kufurushwa inategemea sheria za nchi ambayo walikuwa wamehamia (Marekani),” amesema Kiraithe.

Hatua hiyo imekuja siku chache mara baada ya Rais Donald Trump kuapishwa rasmi kuwa Rais wa nchi hiyo, ambapo amesema jumatano ya leo itakuwa ni siku muhimu kwa usalama wa Marekani, ambapo pia inatarajiwa kuwa ataweka masharti makali kwa raia wa Mataifa saba ya Mashariki ya Kati na Afrika yenye idadi kubwa ya Waislamu wanaotafuta viza za kwenda Marekani.

Mataifa saba ambayo yanayotajwa kuwekewa masharti magumu kwa raia wake kuingia nchini Marekani ni Syria, Iraq, Iran, Libya, Somalia, Sudan na Yemen.

Wakati wa kampeni zake za Urais, Donald Trump, aliahidi kufanyia mageuzi suala la uhamiaji nchini Marekani ikiwemo kuruhusu ujenzi wa ukuta kati ya Mexico na Marekani kwa ajili ya kuzuia wahamiaji haramu na kuwapiga marufuku Waislamu kuingia katika Taifa hilo ikiwa ni sehemu yake ya kupambana na vita dhidi ya ugaidi.

CHANZO: BBC


RAIS DONALD TRUMP AANZA KUWATIMUA WAAFRIKA RAIS DONALD TRUMP AANZA KUWATIMUA WAAFRIKA Reviewed by Unknown on 15:52 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.