ANNE KILANGO MALECELA ATEULIWA KUWA MBUNGE



Na Mwandishi Wetu

Ikiwa ni takribani miezi tisa tangu Rais John Magufuli kutengua uteuzi wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anne Kilango Malecela, kutokana na kile kilichoelezwa kuwa alitoa taarifa za uongo juu ya uwepo wa watumishi hewa mkoani humo, leo Rais Magufuli amemteua tena Malecela kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu jijini Dar es Salaam imesema kwamba Anne Kilango Malecela, ataapishwa kwa mujibu wa taratibu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

April, 2016, Rais Magufuli alitangaza kutengua uteuzi wa viongozi wa Mkoa wa Shinyanga akiwemo Mkuu wa Mkoa, Anne Kilango Malecela (wakati huo) na Katibu Tawala wa Mkoa huo, Abdul Rashid Dachi, kufuatia kutoa taarifa za uongo kuwa Mkoa huo hauna watumishi hewa.

Mbali na kuteuliwa kuwa Mbunge tena wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Malecela amewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Same  Mashariki  na pia Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi katika serikali ya awamu ya nne.
ANNE KILANGO MALECELA ATEULIWA KUWA MBUNGE ANNE KILANGO MALECELA ATEULIWA KUWA MBUNGE Reviewed by Unknown on 20:51 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.