MASHIRIKA YA UTOAJI MIMBA KUNYIMWA MSAADA NA MAREKANI




Rais wa Marekani, Donald Trump, akionyesha sehemu ya maagizo yake aliyotia saini yanayovunja Mpango wa Ushirikiano wa Kiuchumi wa nchi 12 zinazounganishwa na bahari ya Pasifiki (TPP) kama ishara ya kuiondoa Marekani katika mpango huo.
Marekani

Ni wiki yake ya kwanza ofisini tangu alipoapishwa rasmi ijumaa wiki iliyopita, kuwa Rais wa Marekani, Donald Trump, ameanza kazi katika Ikulu ya Marekani kwa kuvunja mikataba ya Mexico City na TPP.

Rais Trump amevunja mkataba wa Mexico City, ambao ulikuwa unaruhusu serikali ya Marekani kutoa fedha kwa mashirika yake mbalimbali ulimwenguni yanayojishughulisha na masuala ya uzazi wa mpango.

Awali Marekani ilikuwa ikitoa fedha zake kwa makundi na mashirika ya kimataifa ambayo yalikuwa yanazitumia kushughulikia ama kujadili utoaji mimba kama njia mojawapo ya uzazi wa mpango.

Vilevile Rais Trump ameiondoa nchi yake kwenye Mpango wa Ushirikiano wa Kiuchumi wa nchi zinazounganishwa na bahari ya Pasifiki.  Makubaliano ya Mpango wa Kibiashara wa nchi zinazounganishwa na bahari ya Pasifiki (TPP), yalijadiliwa na utawala wa Rais aliyemaliza muda wake, Barack Obama.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Ikulu ya Marekani, Sean Spicer, imesema kwamba hatua hiyo iliyochukuliwa na Rais ni ishara kabisa ya kuanza kwa enzi mpya ya sera za kibiashara ya Marekani, ambazo zitakuwa na masilahi mapana kwa Marekani, kwakuwa zitaongeza ushindani wa wafanyakazi wa Marekani pamoja na uzalishaji.

CHANZO: BBC SWAHILI
MASHIRIKA YA UTOAJI MIMBA KUNYIMWA MSAADA NA MAREKANI MASHIRIKA YA UTOAJI MIMBA KUNYIMWA MSAADA NA MAREKANI Reviewed by Unknown on 07:34 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.