MASHUSHU WA MAREKANI NA KENYA WAUWAWA NA AL-SHABAB

Wapiganaji wa kundi la kigaidi la Al-Shabab
Somalia

Kundi la kigaidi la Al-Shabab la nchini Somalia limewaua watu watatu kwa kile linachodai kuwa walikuwa wanalisaidia Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) pamoja na vitengo vyake vingine kulipeleleza kundi hilo.

Watu waliobainika na Al-Shabab kuwa walihusika moja kwa moja kuwachunguzia Maofisa wa Ujasusi wa Marekani na Kenya juu ya mtandao wa kundi hilo, hali iliyosababisha mashambulizi kadha kutekelezwa kwa kutumia ndege zisizo na rubani ni Abdullahi Damey Mohamoud Nur (36), ambaye alikuwa akipokea mshahara wa dola 200 kila mwezi.

Mtu mwingine ni Mohamed Iman Hassan (42), ambaye aliuwawa kwa kuwapelelezea Maofisa wa Shirika la Ujasusi wa Kenya na alikuwa akilipwa mshahara wa dola 150 na Kenya kwa kazi hiyo.

Aidha Mohamed Sharrif Ali (21) ameuwawa kwa kuisaidia Mamlaka ya Jubbaland, ambayo alikuwa anaikusanyia habari mbalimbali kuhusu kundi hilo.

CHANZO: BBC
MASHUSHU WA MAREKANI NA KENYA WAUWAWA NA AL-SHABAB MASHUSHU WA MAREKANI NA KENYA WAUWAWA NA AL-SHABAB Reviewed by Unknown on 15:39 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.