CCM YAMVUA UANACHAMA SOPHIA SIMBA, Dk. Nchimbi na Alhaji Kimbisa waonywa vikali

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), Sophia Simba.

Na Mwandishi wetu

Mwanachama mkongwe wa Chama cha Mapinduzi (CCM), na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake CCM Taifa (UWT), Sophia Simba, leo amevuliwa rasmi uanachama wake ndani ya chama hicho.

Uamuzi huo umekuja wakati wa mkutano mkuu maalumu wa CCM uliofanyika leo mjini Dodoma, ambapo Sophia Simba ametiwa hatiani kwa kukisaliti chama wakati wa uchaguzi mkuu uliokuwa na ushindani mkali mwaka 2015.

Aidha CCM imewapa onyo kali wanachama wengine waliopatikana na hatia ya kukisaliti chama hicho akiwemo Dk. Emmanuel Nchimbi na Alhaji Adam Kimbisa.

Inaelezwa kuwa wanachama hao watatu wametiwa hatiani kwa usaliti kutokana na kile kinachoitwa kumuunga mkono Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, katika mchakato wa kumtafuta mgombea wa Urais kupitia CCM kabla ya kukatwa kwake na kuondoa kwenda kujiunga na Chadema.
CCM YAMVUA UANACHAMA SOPHIA SIMBA, Dk. Nchimbi na Alhaji Kimbisa waonywa vikali CCM YAMVUA UANACHAMA SOPHIA SIMBA, Dk. Nchimbi na Alhaji Kimbisa waonywa vikali Reviewed by Unknown on 14:20 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.