JPM AMTEUA MKE WA KIKWETE KUWA MBUNGE

Mama Salma Kikwete.
Na Mwandishi wetu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli, amemteua mke wa Rais mstaafu awamu ya nne, Dk. Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu imesema kuwa Mama Salma Kikwete ataapishwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zitakazotangazwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hata hivyo awali taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu ilieleza kuwa Mama Salma Kikwete ameteuliwa kama Mbunge wa viti maalumu lakini baadaye taarifa hiyo ilisahihishwa na kueleza kuwa ameteuliwa kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutokana na mamlaka aliyonayo Rais ya kuteua wabunge kumi kwa mujibu wa katiba.
JPM AMTEUA MKE WA KIKWETE KUWA MBUNGE JPM AMTEUA MKE WA KIKWETE KUWA MBUNGE Reviewed by Unknown on 20:24 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.