SERIKALI YAKANUSHA KUFUATILIA MITANDAO YA KIJAMII

Na Mwandishi wetu

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu jijini Dar es Salaam, imekanusha taarifa iliyozagaaa katika mitandao ya kijamii inayosema kuwa serikali inafuatilia kwa karibu mambo yote yanayoendelea katika mitandao ya kijamii na endapo serikali ikibaini hayana tija itaifungia mitandao hiyo kutumika nchini.

Kwa mujibu wa taarifa aliyoitoa Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa kupitia ukurasa wake wa 'Twitter' amesema kuwa taarifa hiyo siyo ya kweli bali imetengenezwa na wahalifu wa mitandao, hivyo amewaomba wananchi kuipuuza mara moja.
SERIKALI YAKANUSHA KUFUATILIA MITANDAO YA KIJAMII SERIKALI YAKANUSHA KUFUATILIA MITANDAO YA KIJAMII Reviewed by Unknown on 14:53 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.