VODACOM YAZINDUA RASMI UUZAJI HISA KWA UMMA


Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom, Ian Ferrao.

Na Mtapa Wilson

Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania PLC leo imezindua rasmi uuzaji wake wa hisa kwa umma kupitia Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), ikiwa ni utekelezaji wa Sheria ya Electroniki na Mawasiliano ya Posta (EPOCA) na Sheria ya Fedha ya mwaka 2016.

Sheria hiyo inaelekeza kampuni za simu kumilikisha asilimia 25 ya hisa zake kwa wananchi kwa kujiunga na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).

Akizungumza katika uzinduzi huo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Vodacom Tanzania PLC, Ian Ferrao, amesema kwamba kampuni yake imeanza rasmi uuzaji wake wa hisa kwa umma kutokana na matakwa ya sheria.

“Hatua hii ni kubwa na inadhihirisha kuwa Vodacom ipo mstari wa mbele katika kutekeleza agizo la kuuza hisa zake kwa umma na inaonyesha jinsi gani ilivyojipanga kuendeleza sekta ya mawasiliano nchini Tanzania katika siku za usoni,” amesema.

Aidha Ferrao amesema uuzaji wa hisa kwa umma kupitia Soko la Hisa utazidi kukuza shughuli za Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), kwa kuwanufaisha watanzania kiuchumi na kukuza uchumi wa nchi kwa ujumla.

Kampuni ya Vodacom Tanzania PLC inatarajia kuuza hisa takribani 560 zenye thamani ya shilingi bilioni 500, ambapo hisa moja itakuwa ikiuzwa kwa shilingi 850.
VODACOM YAZINDUA RASMI UUZAJI HISA KWA UMMA VODACOM YAZINDUA RASMI UUZAJI HISA KWA UMMA Reviewed by Unknown on 18:58 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.