DK. PETER KAFUMU NA VICKY KAMATA, WABWAGA MANYANGA KAMATI YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA

Kutoka kushoto ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, Dk. Dalaly Kafumu na Makamu mwenyekiti wake, Vicky Kamata.

Na Mwandishi wetu

Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, Dk. Dalaly Kafumu, pamoja na Makamu Mwenyekiti wake, Vicky Kamata, wote kwa pamoja leo wamemwandikia barua Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai, wakimuomba kuchia nafasi zao ndani ya kamati hiyo nyeti.

Hata hivyo, katika barua zao hawajabainisha moja kwa moja sababu za kufanya maamuzi hayo isipokuwa wote kwa pamoja wameeleza kufikia maamuzi hayo kwa hiari yao wenyewe. 

Lakini pia wamemshukuru Spika Ndugai kwa ushirikiano mkubwa aliouonyesha kwao kwa kipindi chote walichokuwa viongozi wa kamati hiyo ndani ya Bunge.
DK. PETER KAFUMU NA VICKY KAMATA, WABWAGA MANYANGA KAMATI YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA DK. PETER KAFUMU NA VICKY KAMATA, WABWAGA MANYANGA KAMATI YA VIWANDA, BIASHARA NA MAZINGIRA Reviewed by Unknown on 11:48 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.