WAYAHUDI WATUHUMIWA KUMUUA YESU

Mwanasheria, Dola Indidis.

Na Mwandishi wetu
Dola Indidis ni mwanasheria kutoka Kenya aliyeishtaki Israel kwa kumuua Yesu Kristo.  Anadai hakuipeleka kesi mahakamani kwa misingi ya kidini bali kwa misingi ya Kisheria. Yeye anachoangalia si unabii bali bali ni hatua za kisheria.

Pia amesisitiza ameamua kumtetea Yesu kama mtoto wa Yusufu (fundi seremala) na sio Yesu kama Masihi.

Alipoulizwa mbona ilitabiriwa Yesu atakufa, anasema anafahamu hilo ila hoja sio Yesu kufa, hoja yake ni mchakato uliyotumika kumuua haikuwa sawa kisheria.  Anadai mahakama ilikosea kujiingiza kwenye kesi hiyo.

Anasema Yesu ungehukumiwa kifo kwa kufuata taratibu za kisheria kusingekuwa na shida, ila aliuawa kikatili bila kupewa haki ya kusikilizwa. Wakati Yesu anapelekwa mahakamani (kwa Pilato) tayari alishaanza kusulubiwa kabla hata hukumu haijatoka.

Huo ulikuwa ukiukwaji wa sheria maana mtuhumiwa hawezi kuadhibiwa kabla ya mahakama kujiridhisha kuwa mtu ana hatia.  Anasema Yesu angepata wakili wa kumtetea angeachiwa huru.  Hata kama ilimpasa kufa angeuawa kwa namna nyingine.

Anadai pia Pilato hakuwa na nguvu ya kisheria ya kusikiliza ile kesi na hata yeye alikiri hilo ndio maana akawarudisha wayahudi kwa Herode.  Lakini akalazimishwa kutoa hukumu kwa shinikizo la mfalme Herode.

Pia anadai Pilato alikiri Yesu kutokuwa na hatia, lakini bado alisulubiwa.  Sasa kama Pilato ndio alikuwa Jaji na hakuona hatia ya Yesu kwanini bado Wayahudi walimsulubisha?

Akaongeza kuwa kitendo cha Wayahudi kumsulubisha Yesu mbele ya Jaji (Pilato) ni kujichukulia sheria mkononi na ni uvunjifu wa haki za binadamu.

Anadai misingi ya haki ilikiukwa katika kuongoza kesi (miscarriage of Justice) na Yesu hakupewa nafasi ya kusikilizwa japo alikuwa akilalamika.

Amesema pia kuwa maamuzi hayakuzingatia kanuni za haki ya asili (principle of natural justice), na hukumu inapaswa kurekebishwa na Israel kuomba msamaha.

Ametumia kesi ya Mwai Kibaki vs Daniel Arap Moi yam waka 1999 kama sehemu ya marejeo ya kesi yake (MWAI KIBAKI Vs DANIEL TOROITICH ARAP MOI, Case Number :Civ App 172 of 1999").

Mwanasheria huyo anaungwa mkono na makanisa kutoka nchi za Norway, Marekani, Israel, Uingereza, Tanzania, Afrika Kusini, Canada na Ujerumani.
WAYAHUDI WATUHUMIWA KUMUUA YESU WAYAHUDI WATUHUMIWA KUMUUA YESU Reviewed by Unknown on 12:00 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.