CHADEMA YAFUNGUKA KUKAMATWA TUNDU LISSU

Mwanasheria Mkuu wa Chadema na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.
Na Mwandishi wetu

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Vicent Mashinji, amesema kuwa kwa sasa Taifa linaendeshwa kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na utawala wa sheria, ambapo viongozi waliopewa dhamana wameamua kusigina katiba kwa matakwa yao binafsi.

Dk. Mashinji ametoa kauli hiyo mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, wakati akitoa tamko la chama chake kuhusu kitendo cha Jeshi la Polisi kumkamata Mwanasheria wa chama hicho na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.

Amesema mpaka sasa Jeshi la Polisi limeshindwa kubainisha makosa yaliyosababisha Mbunge huyo kukamatwa na kukimbizwa haraka makao makuu ya polisi, jijini Dar es Salaam kutoka mjini Dodoma, ambako alikuwa anahudhuria vikao vya Bunge vinavyoendelea hivi sasa.

“Kinachofanyika hivi sasa ni ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu na utawala wa sheria.  Haiwezekani na wala haingii akilini Mbunge mwenye dhamana ya kuwakilishi wananchi ndani ya Bunge akamatwe bila kosa." 

"Tumekwenda polisi leo asubuhi kumuona lakini hakuna kosa analoshitakiwa nalo.  Badala yake Polisi wanamtaka atoe maelezo yake aliyoyatoa wakati akiwa katika jimbo la Dimani, mjini Zanzibar,” amesema Dk. Mashinji.

Tundu Lissu alikamatwa na Jeshi la Polisi siku ya jumatatu wiki hii akiwa anatoka kuhudhuria vikao vya Bunge mjini Dodoma, lakini hata hivyo haikuwekwa wazi sababu ya kukamatwa kwakwe.


CHADEMA YAFUNGUKA KUKAMATWA TUNDU LISSU CHADEMA YAFUNGUKA KUKAMATWA TUNDU LISSU Reviewed by Unknown on 15:52 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.