RAIS MAGUFULI: VITA DAWA ZA KULEVYA INAHUSU SERIKALI NZIMA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli.
Na Mwandishi wetu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli amesema kuwa kampeni dhidi ya dawa za kulevya si kampeni ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, peke yake bali ni kampeni ya serikali nzima.
Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati akimuapisha Mkuu mpya wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), Jenerali Venance Mabeyo, ambapo amesema katika kampeni hiyo hakuna atakayepona.
Amesema hata kama mtoto wa Rais anahusika nae akamatwe, hata kama mke wake anahusika nae akamatwe.
Aidha Rais Magufuli ameshangazwa na kitendo cha mmoja wa watu waliokamatwa na dawa za kulevya huko kusini mwa Tanzania mpaka sasa haijukikani kesi yake ilipofikia.
Vilevile Rais Magufuli, amempongeza Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Ernest Mangu, kwa kuwasimamisha kazi askari polisi 12 waliotuhumiwa kujihusisha na mtandao wa biashara ya dawa za kulevya.
Rais Magufuli amemwambia IGP Mangu, kama angekuwa hajawasimamisha kazi askari polisi hao mpaka sasa basi yeye ndiyo angemtumbua.


RAIS MAGUFULI: VITA DAWA ZA KULEVYA INAHUSU SERIKALI NZIMA RAIS MAGUFULI: VITA DAWA ZA KULEVYA INAHUSU SERIKALI NZIMA Reviewed by Unknown on 09:10 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.