KINARA WA ULANGUZI MIHADARATI AKAMATWA
Rais wa Mexico, Enrique Pena Nieto. |
Mexico
Kikosi maalum cha kupambana na biashara ya mihadarati nchini
Mexico kimemtia nguvuni kinara mmoja wa genge la Beltran Leyva, ambalo
hujishughulisha na ulanguzi wa mihadarati katika eneo la Nuevon Leon, kaskazini
mwa nchi hiyo.
Kinara huyo ni Eleazar
Palomo Castillo, maarufu kwa jina la El Cochi au The Pig, ambaye anatajwa kuwa
kama kiongozi mkuu wa mihadarati katika mji wa San Pedro Garza Garcia, na
kamanda msaidizi wa wa genge hilo katika jimbo hilo linalopakana na Marekani.
El Cochi, alikamatwa na vikosi vya Mexico baada ya gari lake
kukataa kusimama katika kizuizi kimoja cha ukaguzi karibu na uwanja wa ndege wa
Monterrey nchini humo.
CHANZO: BBC
KINARA WA ULANGUZI MIHADARATI AKAMATWA
Reviewed by Unknown
on
13:10
Rating:
No comments: