KAMANDA SIRRO: WANAOSHANGAA 'CENTRAL' TUTAWASHUGHULIKIA NA 'TUTAWAGONGA'

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro.
Na Mtapa Wilson

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro, amepiga marufuku kuanzia leo kitendo cha wananchi kwenda kituo kikuu cha polisi maarufu kama 'central' na kukusanyika hovyo nje ya kituo hicho bila kuwa na sababu maalum ikiwemo kuwashangaa watuhumiwa wa mihadarati wanaofika kituoni hapo.

Kamishna Sirro, amesema tabia ya wananchi kukusanyika nje ya kituo kikuu cha polisi imekuwepo tangu kuanza kwa zoezi hilo (juma moja lililopita) la kuitwa kwa watuhumiwa wa biashara na matumizi ya mihadarati, jambo ambalo amelieleza kama tishio kwa usalama wa wananchi wenyewe na Jeshi la Polisi.

“Kumekuwa na tabia ya wananchi kuacha shughuli zao na kukimbia kuja kituo kikuu cha polisi.  Jueni kwamba kituo cha polisi siyo mahala pa kuja kupiga soga, siyo mahala pa kuja kutafutia wachumba.”

“Kituo cha polisi ni mahala unakuja kwa sababu maalum, ukishahudumiwa unaondoka.  Sasa inaonekana kuna watu wanakuja wanajazana kuanzia asubuhi wanakaa wanatafuta chipsi hapahapa na ukimuuliza anachokifanya hata hajui,” amesema Kamishna Sirro.

Aidha Kamishna Sirro, amesema kuwa mtu ambaye anatakiwa kuonekana katika eneo hilo la kituo kikuu cha polisi ni lazima awe na sababu ya msingi, ambapo anapaswa kwenda moja kwa moja kwenye kitengo cha huduma kwa wateja ndani kituo ili asaidiwe shida yake badala ya kukaa nje ya kituo akirandaranda hovyo, jambo ambalo litamfanya achukuliwe hatua kali za kisheria.

“Mahala pa polisi pana mambo mengi ya serikali.  Hatuwezi kuruhusu mtu yeyote anaingia anazunguka, anajichanganya, anakula chipsi, tutamshughulikia na tutamgonga kwa mujibu wa sheria,” amesema Kamanda Sirro. 
KAMANDA SIRRO: WANAOSHANGAA 'CENTRAL' TUTAWASHUGHULIKIA NA 'TUTAWAGONGA' KAMANDA SIRRO: WANAOSHANGAA 'CENTRAL' TUTAWASHUGHULIKIA NA 'TUTAWAGONGA' Reviewed by Unknown on 13:28 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.