CHID BENZ, MR BLUE NA RECHO 'WAMGOMEA' MAKONDA TUHUMA ZA MIHADARATI

Msanii Rashid Makwilo maarufu kama Chid Benz.
Na Mwandishi wetu

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ameliagiza jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam kuendesha msako mkali dhidi ya wahutuhumiwa wa uuzaji, usambazaji na utumiaji wa dawa za kulevya ambao wamekaidi agizo lake la kujisalimisha wenyewe.

Mkuu huyo wa Mkoa, jana alitaja watu ambao wanahusika na biashara hiyo wakiwamo wasanii wa filamu na muziki wa bongo fleva, ambapo aliagiza wajisalimishe wenyewe leo katika kituo kikuu cha polisi jijini Dar es Salaam.

Katika orodha iliyotolewa na Makonda, jana mbele ya wanahabari ilionyesha idadi ya wasanii nane lakini ambao wamefanikiwa kujisalimisha leo kituoni ni wasanii wanne tu ambao ni Wema Sepetu, Khalid Mohamed (TID), Hamidu Chambuso (Nyandu Toz) na Babu wa Kitaa, ambaye pia ni mtangazaji wa kituo cha televisheni cha Clouds.

Miongoni mwa wasanii ambao walitajwa jana lakini wamekaidi wito wa Mkuu huyo wa Mkoa ni Rashid Makwilo (Chid Benz), Heri Samir (Mr Blue) na Winfrida Josephat (Recho), ambapo Makonda ameamuru wasanii hao kusakwa na kuwekwa rumande kwa kutotii amri yake ya kujisalimisha wenyewe leo kituoni.
CHID BENZ, MR BLUE NA RECHO 'WAMGOMEA' MAKONDA TUHUMA ZA MIHADARATI CHID BENZ, MR BLUE NA RECHO 'WAMGOMEA' MAKONDA TUHUMA ZA MIHADARATI Reviewed by Unknown on 18:59 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.