11 MBARONI KWA KUKUTWA NA KETE 38 ZA MIHADARATI NA MAGUNIA SITA YA BANGI

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro.
Na Mtapa Wilson

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kupitia Kamishna Simon Sirro, limesema kuwa limewakamata watuhumiwa 11 wa biashara ya mihadarati, kete 38 za mihadarati pamoja na magunia sita ya bangi, katika operesheni yake maalum ya kupambana ili kuitokomeza kabisa biashara hiyo haram.

Kamishna Sirro ametoa taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, ambapo amewashukuru wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam, kwa ushirikiano wao wa kutoa taarifa za watuhumiwa hao, ambazo zimesaidia kwa kiasi kikubwa kukamatwa kwao.

“Tunaendelea vizuri na operesheni dhidi ya wauza dawa za kulevya pamoja na wavutaji wa dawa hizo.  Niseme tu kwamba jana kuna watuhumiwa 11 wamekamatwa na dawa za kulevya  zipatazo kete 38.  Lakini pia bangi magunia yapatayo sita yamekamatwa.  Kwahiyo operesheni inaendelea vizuri sana.”

"Napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza na kuwashukuru sana wana Dar es Salaam, wanaotupa taarifa kuhusiana na uhalifu wa namna hii,” amesema Kamishna Sirro.
11 MBARONI KWA KUKUTWA NA KETE 38 ZA MIHADARATI NA MAGUNIA SITA YA BANGI 11 MBARONI KWA KUKUTWA NA KETE 38 ZA MIHADARATI NA MAGUNIA SITA YA BANGI Reviewed by Unknown on 12:03 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.