CHUO KIKUU CHA LAGOS MARUFUKU NGUO ZA KUBANA

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Lagos nchini Nigeria (Picha na BBC)
Lagos, Nigeria

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Lagos nchini Nigeria, wamepigwa marufuku kuvaa nguo za kubana mwili kutokana na nguo hizo kuonesha sehemu mbalimbali nyeti za miili yao, jambo ambalo si zuri kwa maadili ya kiafrika.

Tangazo hilo linalokataza hali hiyo limetolewa na uongozi wa chuo hicho, ambapo limeeleza kuwa wanafunzi wanapaswa kuvaa nguo safi tena zinazohifadhi vizuri miili yao badala ya kuwaonesha sehemu nyeti za miili yao kama vile kifua, tumbo, matiti na makalio.

Tatizo la uvaaji usiokuwa na staha miongoni mwa wanafunzi wa vyuo vikuu limekuwa likiongezeka siku hadi siku ikiwamo wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Tanzania, ambapo licha ya kuainishwa kwa misingi na maadili ya uvaaji katika vyuo hivyo lakini bado hali hiyo imeendelea kuwepo.

CHANZO: BBC
CHUO KIKUU CHA LAGOS MARUFUKU NGUO ZA KUBANA CHUO KIKUU CHA LAGOS MARUFUKU NGUO ZA KUBANA Reviewed by Unknown on 06:08 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.