WEMA SEPETU NA WENZAKE WASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA MIHADARATI

Nyota wa filamu na Mshindi wa Ulimbwende nchini Tanzania mwaka 2006, Wema Sepetu.

Na Mwandishi wetu

Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, linawashikilia watu wapatao 17 wakiwamo wasanii maarufu pamoja na askari polisi wa jeshi hilo waliotuhumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuhusika na uuzaji, usambazaji na utumiaji wa dawa za kulevya.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku moja baada ya Mkuu huyo wa Mkoa, kuwataja watuhumiwa kadhaa wakiwamo askari polisi, wasanii wa filamu na muziki wa bongo fleva, ambao wanadaiwa kuhusika na mtandao wa biashara ya dawa za kulevya, ambapo aliwaomba leo wajisalimishe kituo kikuu cha polisi, jijini Dar es Salaam.

Kamanda Sirro amesema operesheni ya kuwakamata watu hao ilianza tangu jana kupitia kikosi maalum kinachohusisha askari polisi na vyombo vingine vya usalama, ambapo watu watano walitiwa mbaroni na kufikisha idadi ya watu waliokamatwa hadi leo kufikia 17.

Baadhi ya watu wanaoshikiliwa na jeshi la polisi mpaka sasa kwa mahojiano ni nyota maarufu wa filamu na aliyewahi kuwa mshindi wa ulimbwende nchini mwaka 2006, Wema Sepetu, Khalid Mohamed (TID), Hamidu Chambuso (Nyandu Toz) na Mtangazaji wa kituo cha televisheni cha Clouds, Babu wa Kitaa, ambao wameitikia wenyewe wito huo wa Mkuu wa Mkoa.
WEMA SEPETU NA WENZAKE WASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA MIHADARATI WEMA SEPETU NA WENZAKE WASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA MIHADARATI Reviewed by Unknown on 17:37 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.