LIPUMBA: SERIKALI ISIKURUPUKE KUPELEKA MAHAKAMANI WATUHUMIWA WA MIHADARATI

Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Prof. Ibrahim Lipumba.
Na Mwandishi wetu
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) anayepingwa na baadhi ya wanachama wa chama hicho, Prof. Ibrahim Lipumba amesema kuwa anaunga mkono suala la watuhumiwa wa biashara au matumizi ya dawa za kulevya kukamatwa.
Prof. Lipumba amesema hayo leo jijini Dar es Salaam, nje ya Mahakama Kuu, alipokuwa amekwenda kusikiliza mwenendo wa mgogoro baina yake na Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad, ambapo amesema anaunga mkono suala la watuhumiwa hao kukamatwa na serikali inapaswa kupongezwa kwa hilo
Aidha Lipumba aliongeza kuwa, serikali isikurupuke kuwapeleka watuhumiwa hao mahakamani bila kuwa na ushahidi wa kutosha kwakuwa suala hilo linaweza kuigharimu fedha nyingi serikali katika uendeshaji wa kesi hizo.
LIPUMBA: SERIKALI ISIKURUPUKE KUPELEKA MAHAKAMANI WATUHUMIWA WA MIHADARATI LIPUMBA: SERIKALI ISIKURUPUKE KUPELEKA MAHAKAMANI WATUHUMIWA WA MIHADARATI Reviewed by Unknown on 16:42 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.