POLISI 12 WALIOTUHUMIWA KWA MIHADARATI WASIMAMISHWA KAZI

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu.
Na Mwandishi wetu

Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu, leo amewasimamisha kazi askari 12 kufuatia tuhuma zilizotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ambaye juzi alitoa orodha inayowataja baadhi ya askari polisi pamoja na wasanii wanaotuhumiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Taarifa iliyotolewa na Makonda ilisema kuwa askari polisi wamekuwa wakishirikiana na wauza dawa za kulevya kwa kupewa rushwa, ambapo wamekuwa wakitoa siri za jeshi hilo pindi linapokuwa likikabiliana na uhalifu huo, jambo ambalo limekuwa likirudisha nyuma juhudi za serikali za kutaka kuitokomeza kabisa biashara hiyo haram.

Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi, amewataja askari polisi waliosimamishwa kazi leo ili kupisha uchunguzi kutokana na tuhuma zinazowakabili ni pamoja na PF 14473 SACP Christopher Fuime, PF 17041 INSP Jacob Hashim Swai, D 3499 D/SGT Steven Apelesi Ndasha, E 8431 D/SGT Mohamed Juma Haima, E 5204 D/SGT Steven John Shaga, E 5860 D/CPL Dotto Steven Mwandambo, E 1090 D/CPL Tausen Lameck Mwambalangani.

Aidha askari wengine waliotajwa kusimamishwa kazi ni E. 9652 D/CPL Benatus Simon Luhaza, D. 8278 D/CPL James Salala, E. 9503 D/CPL Noel Masheula Mwalukuta, WP 5103 D/C Gloria Mallya Massawe na F. 5885 D/C Fadhili Ndahani Mazengo.
POLISI 12 WALIOTUHUMIWA KWA MIHADARATI WASIMAMISHWA KAZI POLISI 12 WALIOTUHUMIWA KWA MIHADARATI WASIMAMISHWA KAZI Reviewed by Unknown on 15:26 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.