RAIS MUGABE KUCHINJA NG'OMBE 150 'BIRTHDAY' YAKE

Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe.
Zimbabwe

Ng’ombe takribani 150 wanatarajiwa kuchinjwa nchini Zimbabwe ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya sherehe kwa ajili siku ya kuzaliwa kwa Rais Robert Mugabe, ambaye anatimiza miaka 93 ifikapo Februari 21, mwaka huu.

Idadi hiyo ya mifugo kwa ajili ya kitoweo inatarajiwa kukusanywa kutoka kwa wakulima wakubwa, ambao walipatiwa mashamba makubwa na serikali baada ya kuyachukua kwa nguvu kutoka kwa Wazungu katika maeneo ya Matebeleland.

Sherehe hiyo ya kuzaliwa kwa Rais Mugabe itafanyika katika eneo la Matobos nje kidogo ya mji wa Bulawayo na inatarajiwa kuhudhuriwa na wananchi wapatao 100,000.

CHANZO: BBC


RAIS MUGABE KUCHINJA NG'OMBE 150 'BIRTHDAY' YAKE RAIS MUGABE KUCHINJA NG'OMBE 150 'BIRTHDAY' YAKE Reviewed by Unknown on 12:20 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.