IRAN: WAMAREKANI SASA RUKSA KUINGIA NCHINI KWANGU

Rais wa Iran, Hassan Rouhani.
Iran

Iran imefuta agizo lake lililokuwa linakataza raia wa Marekani kuingia nchini mwake, ikiwa ni mwendelezo wa majibizano yake na kauli ya Rais Donald Trump wa Marekani, ambaye hivi karibuni aliagiza raia wa Mataifa saba duniani yenye Waislamu wengi kutoingia nchini mwake.

Mamlaka ya mambo ya kigeni nchini Iran, imesema kuwa hatua hiyo imekuja kufuatia uamuzi wa Mahakama uliotolewa jana nchini Marekani na kuamuru kuahirishwa kwa muda agizo la kuwafurusha raia kutoka mataifa hayo saba ikiwamo Iran.

Uamuzi huo wa Iran, utawawezesha sasa wanamichezo wa kikosi cha mieleka wa Marekani, ambao awali walinyimwa viza, kuingia Iran kwa ajili ya kushiriki mashindano ya dunia yatakayofanyika nchini humo baadaye mwezi huu.

CHANZO: BBC


IRAN: WAMAREKANI SASA RUKSA KUINGIA NCHINI KWANGU IRAN: WAMAREKANI SASA RUKSA KUINGIA NCHINI KWANGU Reviewed by Unknown on 12:35 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.