VIGOGO WA MIHADARATI KUTAJWA TENA LEO


Na Mtapa Wilson

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, leo saa nne asubuhi anatarajiwa kutangaza orodha nyingine ya majina ya watu wanaodaiwa kujihusisha na biashara au matumizi ya mihadarati.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Makonda kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram, inasema kuwa awamu ya tatu ya kutaja majina hayo imeshakamilika na ataitaja leo katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.

Hii itakuwa ni mara ya tatu wa Mkuu huyo wa Mkoa kutangaza hadharani majina ya watu wanaotuhumiwa kwa mihadarati baada ya ile ya awali kutaja wasanii kisha kufuatiwa na orodha ya pili iliyotaja watu walioitwa vigogo wa biashara hiyo nchini, ambapo baadhi ya waliotajwa ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, Mfanyabiashara maarufu nchini Yusuph Manji.
VIGOGO WA MIHADARATI KUTAJWA TENA LEO VIGOGO WA MIHADARATI KUTAJWA TENA LEO Reviewed by Unknown on 04:28 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.