NDUGU WA RAIS KOREA KASKAZINI AUAWA

Ndugu wa kambo wa Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong-nam. (AFP)
Kuala Lumpur, Malaysia
Ndugu wa kambo wa Kiongozi Mkuu wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, ameuawa nchini Malaysia, kwa mujibu wa Korea Kusini.
Kim Jong-nam, mwenye umri wa miaka 45, anaripotiwa kulengwa kwenye uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur.
Polisi nchini Malaysia wamethibitisha kwa Shirika la habari la Reuters, kuwa mwanamume raia wa Korea Kaskazini, ambaye alifariki wakati akipelekwa hospitalini kutoka uwanja wa ndege ni Kim.
Kwa mujibu wa ripoti ya televisheni ya Chosum nchini Korea Kusini, Kim aliwekewa sumu akiwa uwanja wa ndege na wanawake wawili wanaoaminiwa kuwa maajenti wa Korea Kaskazini.
Rais wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un. (AFP)
Mwaka 2001, Kim alikamatwa akijaribu kuingia Japan akitumua pasipoti bandia. Aliwaambia maafisa kuwa alikuwa na mpango wa kuzuru eneo la burudani la Disneyland mjini Tokyo.
Kim alikuwa akionekana kama mtu ambaye angemrithi babake lakini kitendo hicho kilisababisha wao kutofautiana.
Kim Jong-nam ndiye mtoto wa kwanza wa kiume wa Kim Jong-il, ambaye aliitawala Korea Kaskazini kuanzia mwaka 1994 hadi wakati wa kifo chake mwaka 2011.
Baada ya nduguye mdogo wa kambo kuchukua uongozi wa Korea Kaskazini wakati babake alipofariki mwaka 2011, Kim Jong-nam hakuoneka sana na alitumia muda wake mwingi nje ya nchi hasa Macau, Singapore na China.
Alinukuliwa na vyombo vya habari vya Japan akisema kuwa alipinga uongozi wa kupokezana.
Pia alinukuliwa na kitabu kimoja mwaka 2012 akisema kuwa mdogo wake ambaye ni nduguye wa kambo hakuwa na tajriba wa kuongoza.
Kim amekuwa akilengwa ili auawe siku za hapo nyuma.  Jasusi mmoja raia wa Korea Kaskazini, ambaye alifungwa nchini Korea Kusini mwaka 2012, aliripotiwa kukiri kuwa alikuwa akipanga njama ya kumuua Kim Jong-nam.
CHANZO: BBC
NDUGU WA RAIS KOREA KASKAZINI AUAWA NDUGU WA RAIS KOREA KASKAZINI AUAWA Reviewed by Unknown on 15:35 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.