KANISA LAPINGA WAUZAJI, WATUMIAJI MIHADARATI KUUWAWA

Rais wa Ufilipino, Rodrigo Duterte.
Ufilipino

Kanisa katoliki nchini Ufilipino limepinga kampeni ya Rais wa nchi hiyo, Rodrigo Duterte, ambayo inalenga kukabiliana na wauzaji pamoja na watumiaji wa dawa za kulevya nchini humo.

Kanisa limesema kuwa kuna upendeleo mkubwa miongoni mwa watu wanaouawa baada ya kubainika kuwa ni wauzaji au watumiaji wa dawa hizo za kulevya.

Mpaka sasa Rais Duterte, ameshaamuru kuuawa kwa kupigwa risasi hadharani maelfu ya watu wanaosadikiwa kufanya biashara ya dawa za kulevya pamoja na watumiaji wa dawa za kulevya nchini Ufilipino, jambo ambalo limekuwa likipigiwa kelele kama ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu.

Ujumbe wa kanisa umesomwa leo jumapili kote nchini Ufilipino.

Lakini hata hivyo ujumbe huo umekuja ikiwa ni siku kadhaa tangu Rais Duterte, asimamishe kwa muda kampeni yake hiyo, kutokana na ufisadi uliopo katika idara ya polisi, jambo ambalo analitaja kama kikwazo kinachohujumu juhudi zake za kumaliza kabisa biashara ya mihadarati nchini mwake.

CHANZO: BBC 
KANISA LAPINGA WAUZAJI, WATUMIAJI MIHADARATI KUUWAWA KANISA LAPINGA WAUZAJI, WATUMIAJI MIHADARATI KUUWAWA Reviewed by Unknown on 13:57 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.