CHADEMA YANG'AKA MBOWE KUTAJWA DAWA ZA KULEVYA

Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe.
Na Mwandishi wetu

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kupitia Katibu Mkuu, Dk. Vicent Mashinji, kimelaani vikali kitendo cha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, kumtaja Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, kama mmoja wa vigogo wanaotuhumiwa kwa biashara ya mihadarati.

Akijibu swali lililoulizwa na mwandishi wa habari wa gazeti la Habari Leo, ambaye alitaka kujua ni ipi kauli ya chadema kuhusiana na orodha iliyotolewa na Makonda ambayo ndani yake jina la Mwenyekiti wa chama hicho limetajwa.

Dk. Mashinji amesema kuwa kitendo hicho ni mwendelezo wa hujuma dhidi ya upinzani, ambapo toka mwanzo viongozi wa ngazi za juu serikalini walinuwia kuumaliza kabisa upinzani kabla ya uchaguzi wa mwaka 2020.

“Suala hili ni tuhuma za mtu binafsi.  Ila kitu ambacho naweza kusema ni kwamba, tunalaani sana kitendo hiki kwakuwa ni udhalilishaji mkubwa wa Mwenyekiti wetu, ambaye ni Kiongozi Mkuu wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni, nafasi ambayo ni sawa na Waziri Mkuu.”

“Kumtaja kwa namna hiyo bila kuwa na ushahidi dhahiri ni kumdhalilisha.  Toka serikali hii imeingia madarakani imeshafanya mambo mengi kwa Mbowe na kila mtu anajua.  Ila ninachoamini na jinsi ninavyomfahamu Mbowe ataendelea kusimama imara kama alivyosimama imara tangu awali.  Katika suala hili ninaamini kabisa Mbowe mwenyewe atalieleza,” amesema Dk. Mashinji.

Leo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ametoa orodha mpya ya watu 65, ambao wanatuhumiwa kujihusisha na biashara ya mihadarati, ambayo ndani yake amewataja wanasiasa na wafanyabiashara maarufu pamoja na kiongozi wa kiroho wa kanisa la Uzima na Ufufuo, Josephat Gwajima.
CHADEMA YANG'AKA MBOWE KUTAJWA DAWA ZA KULEVYA CHADEMA YANG'AKA MBOWE KUTAJWA DAWA ZA KULEVYA Reviewed by Unknown on 16:52 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.