MAHAKAMA YARUHUSU WAISLAMU KUINGIA MAREKANI

Rais wa Marekani, Donald Trump.
Marekani

Mashirika ya ndege mbalimbali sasa yataanza kubeba abiria kutoka Mataifa saba yenye Waislamu wengi, ambayo awali raia wake walipigwa marufuku kuingia Marekani.

Kauli hiyo imetolewa leo na Idara ya Forodha ya Marekani, ambayo imeruhusu sasa abiria kutoka Mataifa hayo saba kuingia nchini Marekani.

Hali hiyo imekuja ikiwa ni saa chache baada ya Jaji wa Mahakama ya Taifa ya Marekani kuzuia amri ya Rais Donald Trump, ambaye alitaka raia wa Mataifa hayo saba, ambayo yana Waislamu wengi kutoingia nchini mwake.

Mahakama iliamua kuwa Rais Trump, alivunja katiba, ambayo inakataza dini moja kupendelewa kuliko dini nyingine. 

Lakini hata hivyo serikali imesema itakata rufaa kupinga hukumu hiyo ya Mahakama kwani Rais Trump ameendelea kusisitiza kuwa hatua yake hiyo imekusudia kuwalinda Wamarekani.

Mataifa saba ambayo raia wake walizuiliwa kuingia Marekani ni Syria, Iraq, Iran, Libya, Somalia, Sudan na Yemen.

CHANZO: BBC


MAHAKAMA YARUHUSU WAISLAMU KUINGIA MAREKANI MAHAKAMA YARUHUSU WAISLAMU KUINGIA MAREKANI Reviewed by Unknown on 18:36 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.