SERIKALI YAIONYA MWANAHALISI


Mwandishi wetu

Serikali imelionya gazeti la Mwanahalisi kutokana na kitendo chake cha kuchapisha taarifa zinazodaiwa kuwa ni uzushi na kuahidi kuwa itachukua hatua kali zaidi endapo gazeti hilo litaendelea na uandishi huo unaokiuka maadili ya kitaaluma pamoja na sheria za nchi.

Hatua hiyo imekuja siku moja baada ya gazeti hilo kuomba radhi kwa kitendo chake cha kuchapisha habari iliyokuwa inasomeka kuwa “UFISADI NDANI YA OFISI YA JPM”, jambo lililotafsiriwa kama kumuhusisha Rais Magufuli na ufisadi huo, wakati habari ilikuwa inahusu ufisadi uliofanyika katika Shirika la Elimu Kibaha.

Aidha taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo, Hassan Abbasi, imemuagiza Mhariri wa Mwanahalisi, Jabir Idrissa, kuchapisha barua yake ya kuomba radhi katika ukurasa wa mbele wa gazeti hilo katika toleo lijalo la Februari 6, 2017, kwakuwa habari husika ilichapishwa katika ukurasa wa mbele wa gazeti hilo toleo lililopita. 
SERIKALI YAIONYA MWANAHALISI SERIKALI YAIONYA MWANAHALISI Reviewed by Unknown on 15:23 Rating: 5

No comments:

Theme images by merrymoonmary. Powered by Blogger.